Taifa Leo
327 FOLLOWERS
The only Kiswahili newspaper in Kenya. Topics covered are politics, games, poetry, hybrid news, and more.
Taifa Leo
1h ago
NA WANDERI KAMAU MIONGO kadhaa iliyopita, ilikuwa vigumu sana kumsikia mtu akizungumzia suala la mabadiliko ya hali ya hewa. Lilikuwa suala geni, kwani athari zake hazikuwa zimeanza kudhihirika. Nyakati hizo, maeneo mengi nchini bado yalikuwa na kiwango kikubwa cha misitu. Mito ilikuwa yenye maji mengi na safi yaliyokuwa yakitumika na wanavijiji kwa shughuli zao za ..read more
Taifa Leo
2h ago
NA MERCY KOSKEI RAIS William Ruto Jumanne alitembelea eneo la mkasa Maai Maahiu na kuamuru wanajeshi waungane na kikosi cha kuisaka miili ya walioangamizwa na mafuriko. Rais pia alisema watu wanaoishi eneo hilo, ambalo limeshatambuliwa kuwa hatari, watalazimika kuondoka kuanzia Jumatano, ili kuokoa maisha. “Watu wote wanaoishi katika maeneo haya watalazimika kuondoka ndani ya saa ..read more
Taifa Leo
2h ago
HASSAN WANZALA Na STANLEY NGOTHO PAPA Francis amesema Jumatano kuwa ameguswa na Wakenya kipindi hiki wakikabiliana na mafuriko ya maafa. Kupitia ukurasa wake katika mtandao wa X (zamani Twitter) kiongozi huyo wa kidini ametoa wito wa maombi maalum kwa waathiriwa wa janga hili la kiasili. “Ninafuatilia kwa karibu yanayojiri nchini Kenya kipindi hiki raia wakikabiliana na ..read more
Taifa Leo
4h ago
NA MASHIRIKA MAFURIKO, radi na dhoruba yanaendelea kuhangaisha walimwengu mvua kubwa ikishuhudiwa katika nchi mbalimbali. Wengi wamelazimika kuhama makazi yao kutafuta maeneo salama huku maelfu wakiendelea kupata matibabu. Kwa sasa, nchi kadhaa zikiwemo China, Pakistan, Rwanda, Kenya, Tanzania, Italia, Slovenia na Ugiriki zinakabiliwa na mafuriko. Japo idadi kamili ya vifo duniani havijabainishwa, inakadiriwa kuwa mafuriko ..read more
Taifa Leo
4h ago
NA CHARLES WASONGA VIONGOZI wa kidini wameitaka serikali kuhakikisha kuwa makamishna wapya wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) wanateuliwa kwa wakati ufaao. Kwenye taarifa iliyotolewa baada ya kukamilika kwa Kongamano la Kitaifa la Mazungumzo katika jumba la Ufungamano, Nairobi, walisema si sawa kwa taifa kusalia kwa miezi 16 bila tume halali ya kuendesha ..read more
Taifa Leo
6h ago
NA PETER CHANGTOEK JANGA la ugonjwa wa Covid-19 lilipoanza na kisha kusambaa katika nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, biashara na shughuli nyingine za watu kujitafutia riziki ziliathirika mno. Watu wengi walifutwa kazi katika kampuni tofauti, huku wengine wakilazimika kufanyia kazi nyumbani kwao. Miongoni mwa wale walioathirika ni George Rotich,30. Hata hivyo, ujio wa ugonjwa huo ulimfaidi ..read more
Taifa Leo
6h ago
NA KALUME KAZUNGU MWAMBAO wa Pwani unafahamika sana kwa kuwa na msitu wa mikoko kutokana na kwamba eneo hilo linapakana na Bahari Hindi. Ikumbukwe kuwa mikoko ni aina za miti au vichaka vinavyokua katika maji ya chumvi, hasa kwenye fukwe za bahari za kanda za trokipi. Kwa wale waliobahatika kuujua mkoko wanafahamu fika kuwa mti huo ..read more
Taifa Leo
7h ago
NA DAVID MUCHUNGUH MVUTANO unatokota katika shule ya kitaifa ya Mang’u High kati ya mwalimu mkuu na wazazi wanaomtuhumu kwa kuongeza karo kiholela na kuendesha hoteli ya kibinafsi shuleni miongoni mwa tuhuma nyingine. Kulingana na stakabadhi ambazo Taifa Leo imeziona, mwenyekiti wa Muungano wa Wazazi shuleni humo, Bw Benson Mwenje, amewasilisha kesi kortini kutaka mwalimu mkuu ..read more
Taifa Leo
9h ago
NA OSCAR KAKAI KUFUATIA mvua kubwa inayoendelea kunyesha nchini, kiwango cha maji katika bwawa la Turkwel katika kaunti ya Pokot Magharibi, kinaendelea kuongezeka huku wakazi wakianza kuingiwa na hofu. Wakazi hao wanahofu kuwa huenda bwawa hilo likajaa na kutapika maji, hali inayoweza kusababisha mafuriko ya madhara Pokot Magharibi. Kwa mara ya kwanza mnamo Oktoba 2020 ..read more
Taifa Leo
10h ago
NA GEORGE ODIWUOR WAZAZI na nduguze Joseph Ochoro walikuwa na furaha sana waliposikia angejiunga na Idara ya Magereza. Ulikuwa mwaka wa 2019 wakati alishiriki zoezi la usajili wa makurutu mjini Homa Bay na akafuzu. Alipokea mafunzo Ruiru, Kaunti ya Kiambu na akafaulu kuwa askari jela katika gereza la Nyahururu kuanzia mwaka 2020. Taifa Leo ilipomtembelea ..read more