ALVIN HABARI
50 FOLLOWERS
News, story, music, health, food, politics, education, love etc. All are found here.
ALVIN HABARI
4y ago
KWANINI REAL MADRID WAMEHAMA SANTIAGO BERNABEU?!.
.
Kama umegundua siku za hivi karibuni tangu baada ya Corona michezo ya Real Madrid ya nyumbani imekua ikichezwa katika uwanja wa Estadio Alfredo Di Stefano na sio Santiago Bernabeu kama ilivyozoeleka.
.
Kumeelezwa sababu nyingi na wengi wakiamini kuzuiwa mashabiki kuingia uwanja kuliwafanya Madrid kuacha kuutumia Bernabeu kuepuka gharama za matengenezo kila baada ya mechi,na wakaona labda kutumia Di Stefano itawasaidia katika gharama.
.
Lakini ukweli ni kwamba Bernabeu upo katika matengenezo na maboresho makubwa ambayo yatachukua muda,taarifa ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Dalili Na Tiba Ya Mfadhaiko (DEPRESSION)
Maana Ya Mfadhaiko Wa Akili (Depression)
Kila mmoja wetu ameshapata kuwa na huzuni wakati fulani, ni kitu cha kawaida kinachotokea wakati umepotelewa na kitu, kutokana na mihangaiko ya maisha au kutokana na kudharauiliwa. Huzuni ikizidi na ikienda kwa siku nyingi mfululizo (wiki mbili au zaidi) na ikiambatana na hali ya kujiona kuwa si wa thamani tena, kwamba ni mtu usiye na msaada wo wote – basi hii inaweza kuwa ni zaidi ya huzuni. Unaweza kuwa umepata tatizo la kiafya – mfadhaiko, ugonjwa ambao kwa bahati nzuri una tiba ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Ni Nini Maana Ya Panic Attack? Utakabiliana Vipi Na Panic Attack?
“Ghafla nilisikia wimbi la hofu likitambaa mwilini bila sababu yo yote ile. Moyo wangu ulienda kasi sana, kifua kiliuma na ikawa inazidi kuwa ngumu zaidi kupumua. Nilifikiri kuwa muda wangu wa kufa ulikuwa umewadia.”
Hii ni mfano wa sentensi inayotoka kinywani mwa mtu mwenye tatizo la panic attack. Panic attack inaweza kuelezewa kuwa ni kipindi kifupi cha mtu kukamatwa na hofu kubwa na wasiwasi vinavyokuja ghafla. Moyo ghafla unakwenda mbio na unashindwa kupumua. Unaweza pia kufikiria unakufa au unapata wazimu.
Panic attacks ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Kamanda akanyamaza na
kututazama. Kikapita kimya kifupi
kabla ya kukitanzua kimya hicho.
“Sasa andikisha maelezo yake,
yatawekwa kwenye faili la
marehemu pamoja na maelezo
yenu nyote” Kamanda
akamwambia Inspekta na
kunigeukia mimi.
“Wewe utatupeleka katika hilo
eneo, tutachukua mpiga picha”
akaniambia.
Wakati Inspekta anachukua
maelezo ya yule mwananchi,
kamanda wa polisi na afisa
upelelezi walitoka nje ya kituo
wakakikagua tena kiwiliwili cha
Sajenti Erick kabla ya kuamuru
kipelekwe hospitali kwa uchunguzi
zaidi.
Baada ya hapo aliitwa mpiga picha
wa polisi. Dakika chache baadaye
kamanda wa p ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Sote tukasimama. Kila polisi
akachukua bunduki yake.
Tulishindwa hata kujibu, tukawa
tunatazamana.
“Vipi jamani, mbona mmelala
hapa” Inspekta Amour akatuuliza
tena.
Polisi mmoja akaeleza
kilichotutokea. Polisi hao waliokuja
wakashangaa.
Waliusogelea mwili wa Sajenti Erick
na kuutazama.
“Huyu ndiye Sajenti Erick” Amour
akasema baada ya kuutazama
mwili huo. Akaongeza.
“Sasa nini kilitokea?”
“Ni miujiza mitupu” nilijibu mimi.
“Hiyo nyumba imetowekaje?”
“Hatujui. Muda huu tunazinduka
tunaona nyumba haipo”
“Ilikuwa kwa wapi”
“Sisi tulikuwa uani mwa hiyo
nyumba. Lile gari tulilokuja nalo
lilikuwa m ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Baada ya kumaliza maelezo yake
ambayo yaliwashangaza maafisa
hao, kamanda wa polisi akataka na
mimi nieleze kilichotokea.
“Kwanza ulifikaje katika eneo hilo
na ulikuwa na Sajenti Erick au
ulikuwa peke yako?” akaniuliza.
“Nilikwenda peke yangu” nilimjibu.
“Kufuata nini?”
Niliona kama nitauma uma
maneno nitajikuta nikiwekwa
ndani, jambo la msingi ni kueleza
ukweli wote.
“Kuna msichana niliwasiliana naye
kwenye simu akataka nimfuate
katika eneo hilo”
“Ni nani?”
“Wakati tunawasiliana nilikuwa
simjui lakini baadaye niligundua
alikuwa ni yule msichana ambaye
mama yake tulimshitaki kwa
kukutwa na ke ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Maimuna alikuwa ameshika ule
upanga wake akiangaza macho
yake huku na huku. Sikuweza tena
kusubiri, nikatoka mbio. Nilielekea
upande ule lilikoelekea gari la
polisi.
Wakaniona!
“Si yule!” niliisikia sauti ya
Maimuna.
“Twende tumfuate” Sauti ya kiume
nayo ikasikika.
Niliendelea kukimbia. Kila
nilipopiga hatua tatu nilitazama
nyuma. Niliwaona wananifuata.
Hawakuwa wakikimbia lakini
walikuwa wanakuja kwa haraka.
Kwa mbali nikaona mwanga wa
gari linalokuja. Nikazidi kukimbia.
Niliona nikimbie nikiwa katikati ya
barabara ili watu waliomo ndani ya
gari hilo waweze kuniona.
Nikajitokeza katikati ya ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Mwili na kichwa vimeondolewa.
Nafikiri vimezikwa uani”
nikaongezea maelezo.
“Tumekuta makaburi uani!” Polisi
mwingine akasema.
“”Kwenye hivi vyumba vingine
hamkukuta watu?” Koplo akauliza.
“Hakuna mtu humu ndani. Hii
nyumba iko tupu”
“Hebu twendeni tukayaone hayo
makaburi”
Tukaenda uani. Lile kaburi
nililoliona likichimbwa na yule
mwanamke lilikuwa limefukiwa.
Pembeni yake kulichimbwa kaburi
jingine lililokuwa wazi. Shepe
lilikuwa limeachwa kwenye chuguu
ya mchanga.
“Hili kaburi lililofukiwa ndilo
nililokuta linachimbwa. Bila shaka
mwili wa Sajenti Erick umezikwa
hapa” nikawambia wenzangu.
“T ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Leo nimekwisha!” nikajiambia.
Nilikuwa sina pa kukimbilia. Lakini
nilikwishatambua kila kitu.
Sikujua niliwezaje kuwasiliana na
yule msichana hadi nikafika katika
nyumba ile ya mauti! Kusema kweli
nilijipeleka mwenyewe!
Kwa vyovyote vile, nilijiambia,
nyumba ile haikuwa ya binaadamu
wa kawaida. Yule bibi alikuwa jini!
Na kama alikuwa jini, niliendelea
kujiambia, sitaweza kunusurika mle
ndani.
Licha ya kutoka pale uani, yule bibi
hakushituka. Aliendelea kuchimba
lile shimo kwa bidii.
Hakuna binaadamu yeyote
anayekubali kufa kirahisi,
nikageuka haraka na kurudi
nilikotoka. Wakati nafika kwenye ..read more
ALVIN HABARI
4y ago
Nikajiambia yeye ndiye aliyestahili
adhabu aliyoipata lakini mimi
nilikuwa naonewa tu. Nikaapa
kimoyomoyo kama nitasalimika
sitarudia tena kushirikiana na polisi
wasio waaminifu.
Kwa vile nilikuwa hoi, nikaanguka
chini na kupotewa na fahamu.
Nikiwa sijielewi niliota nainuliwa
na mtu aliyenikuta nimeanguka.
“Mbona umelala hapa?” akaniuliza.
“Nlinguka nilikuwa nakimbia”
nikamjibu.
“Oh pole sana. Ulikuwa unakimbia
nini?”
Nikamueleza ule mkasa
ulionitokea.
“Kwani wewe ulikuwa hujui kama
yule bibi na mwanawe Maimuna ni
majini?”
“Nilikuwa sijui. Kumbe majini
wanaishi na binaadamu?”
“Ndio, wanaishi ..read more